31st August, 2018
Wanafunzi watatu wanazuiliwa na polisi huko nyakach kaunti ya kisumu baada ya kudaiwa kumuua mwalimu wa shule ya upili. Wawili kati ya wanafunzi hao ni wa shule ya upili huku mmoja akiwa wa chuo kikuu. Inasemekana kuwa wanafunzi hao walimchapa mwalimu huyo jina la manase ongole kwa kutumia kifaa butu hadi akafa kutokana na kuvunja damu kupita kiasi .wawili waliokuwa na mwalimu huyo vile vile walijeruhiwa na sasa wanapokea matibabu hospitalini. Haya yalijiri baada ya kurushiana cheche za maneno kwenye eneo moja la burudani huko nyakach eneo la masoko la nyamaroka. wanafunzi hao watapelekwa mahakamani na kushtakiwa kwa tuhuma za mauaji.