×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Madai ya ubakaji Moi girls

31st August, 2018

Uchunguzi kuhusiana na madai ya ubakaji wa mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule ya wasichana ya moi miezi mitatu iliyopita umeendelea kuzingirwa na kizungumkuti baada ya aliyekuwa mwalimu mkuu wa shule hiyo rael muriithi kutetea uwezekano wa tendo hilo kutokea akisisitiza kwamba kumekuwa na usalama wa kutosha kuwadhibiti wanafunzi hao dhidi ya matukio ya aina hiyo. Hata hivyo muriithi amekwepa kudokeza iwapo anao ufahamu wowote kuhusiana na mshukiwa wa tendo hilo akisistiza kwamba suala hilo lingali linachunguzwa na vitengo husika. Aidha usimamizi wa kampuni ya usalama ya lavingtone sawa na mlinzi aliyekuwa kwenye zamu siku ya kisirani hicho wamesimama kidete kwamba usiku unaodaiwa kutokea tendo hilo hawakuona jambo lolote geni na kwamba usalama ulikuwa shwari.

.
RELATED VIDEOS