30th August, 2018
Watoto watatu wa familia moja katika kijiji cha obipor eneo bunge la teso kusini kaunti ya busia wamekumbwa na ugonjwa usiojulikana.wazazi wa watoto hao wameeleza kuwa mmoja wa mtoto wao aliye na umri wa miaka kumi na minane na wawili pacha walio na umri wa miaka kumi na miwili walizaliwa wakiwa na afya nzuri lakini walipofika umri wa miaka mitano wakaanza kupooza katika mazingira ya kutatanisha. Wanasema watoto hao walipokea chanjo zote zinazohitajika ikiwemo chanjo ya ugonjwa wa kupooza au polio. Kwa mujibu wa mtaalamu wa maswala ya viungo katika hosipitali ndogo ya rufaa ya alupe, jude taabu amesema kuwa ulemavu unaowakumba watoto hao unahitaji matibabu ya hali ya juu.