30th August, 2018
Chama cha walimu nchini KNUT kimesitisha mgomo wake kwa sasa ambao ulikuwa ufanyike septemba mosi ili kutoa nafasi ya kufanya mazungumzo na tume ya kuwaajiri walimu tsc kuhusu sera zilizowekwa na ambazo chama hicho kinadai zinahujumu utendakazi wa walimu. Akizungumza katika kaunti ya nyamira, katibu mkuu wa knut wilson sossion ameapa kuwaongoza walimu wote katika maandamano kati ya tarehe 30 mwezi septemba hadi tarehe 5 oktoba iwapo mazungumzo kati ya chama hicho na tsc hayatazaa matunda.