30th August, 2018
Waziri mkuu wa uingereza Theresa May yuko nchini kwa ziara ya siku moja katika ziara inayochukuliwa kuwa muhimu zaidi katika uhusiano wa kibiashara kati ya uingereza na kenya. Ni mara ya kwanza katika kipindi cha miaka thelathini tangu waziri mkuu wa uingereza kuizuru kenya. May yuko katika ziara ya mataifa matatu ya afrika na yuko kenya baada ya kuzuru afrika kusini. Ziara hii inakuja muda mfupi kabla ya uingereza kujiondoa rasmi katika umoja wa ulaya EU.