27th August, 2018
Dalili ya kuchipuka kwa miungano mipya ya kisiasa imeanza kushuhudiwa kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2022 huku gavana wa kaunti ya mombasa hassan joho akielekeza macho yake katika eneo la bonde la ufa. Baada ya kukutana na rais mstaafu daniel moi, mwishoni mwa juma joho amekuwa na misururu ya mikutano katika maeneo mbali mbali ya bonde la ufa akitoa wito kwa wakenya kuwapuuza wanasiasa wanaohusishwa na ufisadi na ubadhirfu wa pesa za umma.