27th August, 2018
Mwenyekiti wa tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC Wafula Chebukati amesimama kidete na kusema waliokuwa makamishna wa tume hiyo, ambao walijiuzulu, hawana shughuli zozote za kutekeleza katika ofisi hiyo. Chebukati aliyezungumza na wanahabari katika jengo la anniversary tower mapema leo, amesema kwamba ni vyema kwa wakenya hao kufahamu kwamba walivyofanya kwa kutangaza hadharani kujiuzulu kwao, kulimaanisha hawapo ofisini tena, na kwamba kujaribu kurudi ofisini kwa mlango wa nyuma ni kinyume cha sheria na ukiukaji wa sura ya sita ya katiba kuhusiana na uadilifu.