26th August, 2018
Naibu Gavana wa mombasa, wabunge wawili na shirika la haki africa sasa wanataka nchi ya uganda kukombolewa kwakile wanachotaja kama uongozi wa kiimla baada ya kukamatwa na kuzuiliwa kwa mwanamuziki mashuhuri ambaye pia ni mbunge Robert Kyagulanyi, maarufu kama bobi wine. viongozi hao wamesema kuwa ikiwa hatua hazitachukuliwa huenda tatizo hilo likaenea maeneo mengine afrika. walizungumza hivi leo katika mkesha wa kuwasha mishuma ya kumkumbuka Bobi Wine.