×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Wanaharakati watishia kushtaki Bunge la kaunti ya Bungoma kwa madai ya ufisadi

25th August, 2018

Wanaharakati wa shirika la kijamii katika Kaunti ya Bungoma wametishia kuelekea kortini kushtaki Bunge la Kaunti hiyo kwa ubadhirifu wa fedha .Hii ni baada ya bunge la Kaunti hiyo kushindwa kuwajibika katika kazi yao ya kuchunguza jinsi fedha zinavyotumika katika bunge hilo. 

Kulingana na stakabadhi zinazodaiwa kuwa ushahidi kuonyesha jinsi ubadhirifu unavyoendelezwa kati ya karani wa bunge John Mosongo akishirikiana na waakilishi wadi katika bunge hilo, wanaharakati hao wanadai kuwa hawana imani na bunge hilo kwa mambo ya uwazi na uwajibikaji ndiposa wameamua kwenda kortini kwa niaba ya wakaazi wa Kaunti ya Bungoma.


Wamevitaka vitengo husika ikiwemo tume ya kupambana NA ufisadi  EACC na ofisi ya kiongozi wa mashtaka ya umma kuingilia kati

.
RELATED VIDEOS