24th August, 2018
Hatimaye shughuli ya usafirishaji wa mafuta kutoka eneo la Lokichar kaunti ya Turkana hadi kaunti ya Mombasa imerejea.
Hii ni baada ya msururu wa mikutano kati ya wakazi wa maeneo Turkana kusini na mashariki sawa na baadhi ya viongozi akiwemo waziri wa madini na petroli John Munyes.