23rd August, 2018
Wenyeji katika eneo la Ongata Rongai kaunti ya Kajiado, wanalalamikia muda mrefu unaotumiwa kutengeneza barabara ya kataka.
Barabara hiyo ambayo kwa sasa iko katika hali duni ilikuwa itengenezwe kutoka eneo la Ongata Rongai hadi Embulbul.
Wahudumu wa pikipiki pamoja na madereva wa magari wanalalama kuwa hali mbaya ya bara bara hiyo inawaharibia magari pamoja na pikipiki. Umbali unaofaa kutengenezwa ni wa zaidi ya kilomita kumi na moja.