22nd August, 2018
Jamii ya Waislamu huko Malindi imemshutumu kiongozi wa wengi bungeni Aden Duale kwa kuingilia masuala ya dini. Imamu wa msikiti wa Jamia huko Malindi Sheikh Feisal Mohamed Alamoudy, aliyesimamia ibada ya siku kuu ya Eid Al Adha hapo jana, amesema kwamba si vyema kumuingilia Kadhi mkuu kwenye masuala ya dini na hivyo kumtaka Duale kukoma kuendeleza semi zinazoonekana kukosa heshima kwa uongozi wa dini.