20th August, 2018
Mji mkuu wa Uganda, Kampala umeshuhudia vurugu hivi leo
baada ya jeshi pamoja na polisi kufyatua risasi za moto
pamoja na mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya wafuasi
wa mbunge wa upinzani Robert Kyagulanyi Ssentamu
almaarufu Bobi Wine. Wafuasi hao wamezua vurugu na
kufunga baraba katika mji wa kampala kulalamikia hatua ya
serikali kuendelea kumzuilia Bobi wine ambaye amefunguliwa
mashtaka ya uhaini