17th August, 2018
Ni afueni kwa Gavana wa Embu Martin Wambora baada ya mahakama ya rufaa kubatilisha uamuzi wa mahakama kuu na kushikilia kuwa ndiye aliyeshinda kiti hicho katika uchaguzi wa mwaka jana. Wambora aliwasilisha ombi lake katika mahakama ya rufaa baada ya ushindi wake kufutiliwa mbali na mahakam kuu tarehe kumi na tisa mwezi septemba mwaka jana. Ushindi wake ulikuwa unatiliwa shaka na mwanasiasa Lenny Kivuti.