7th August, 2018
Wafanyikazi wa kampuni ya ujenzi wa barabara ya chiko kutoka china katika maeneo ya maili kumi, solai na subukia wamefanya maandamano kulalamikia kile wanachosema kuwa ni kunyanyaswa na kuhangaishwa na wasimamizi wa kampuni hiyo. Wafanyikazi hao wamesema kuwa kampuni hiyo imekataa kuheshimu mkataba wa maelewano na vyama vyao vya wafanyikazi na wenzao wamekuwa wakifutwa kazi bila notisi. Wasimamizi wa kampuni hiyo hawakupatikana mara moja kujibu shutuma hizo.