7th August, 2018
Wafugaji katika eneo la Samburu wanakadiria hasara baada ya kukosa soko la kuuza mifugo wao. Wafugaji hao wamesema soko la mifugo limeporomoka baada ya mawakala kukoma kuja kununua mifugo wao. Sasa wafugaji hao wanalazimika kutembea zaidi ya kilomita mia moja kutoka maeneo ya baragoi kutafuta soko la kuuza ng'ombe wao.