6th August, 2018
Wakenya milioni mbili wanakabiliwa na hatari ya kupofuka kutokana na mzozo wa uagizaji wa dawa za thamani ya shilingi bilioni nne zilizotolewa kama msaada na shirika moja nchini marekani. Taarifa zinasema dawa hizo zinazopaswa kuwasaidia watu maskini katika 12 zimekuwa zikizuiliwa katika uwanja wa ndege wa jomo kenyatta kwa kipindi cha miezi kumi baada ya serikali kuchelewa kuidhinisha dawa hizo kuingizwa humu nchini.