27th July, 2018
Zaidi ya familia 100 katika kijiji cha siyu kaunti ya Lamu zinakadiria hasara baada ya takriban minazi 250 kukatwa ili kutoa nafasi ya ujenzi wa barabara itakayounganisha kijiji hicho na eneo la shanga. Wakaazi hao ambao wamejawa na hasira wameilaumu serikali kwa kutowahusisha katika mipango ya ujenzi huo na badala yake waligutushwa tu kuona minazi yao imekatwa wakati wakienda shambani.