17th July, 2018
Maswala ya sanaa na eneo la Garissa kaskazini mwa nchi kwa siku nyingi limekuwa likizingatiwa kuwa mojawepo ya maeneo hatari kutokana na mashambulizi ya mara kwa mara ya kundi la kigaidi la alshabaab. Wengi wamekuwa wakiliepuka eneo hilo. Lakini Msanii wa nyimbo za Ohangla Emma Jalamo anataka kubadilisha dhana hiyo, amekuwa katika mji wa garissa kuwatumbuiza mashabiki kwa nyimbo zake.