13th July, 2018
Rais Uhuru Kenyatta adhuhuri ya leo alisimamia na kushuhudia kiapo cha makamanda wa vikosi vya jeshi, waliopandishwa madaraja katika vikosi vya jeshi la nchi kavu, jeshi la angani na kile kikosi cha majini. Kwa mara ya kwanza, jeshi la kenya limempata mwanamke wa kwanza katika daraja la meja jenerali, ambapo Fatuma Ahmed amepandishwa daraja hadi kwenye ngazi hiyo.