12th July, 2018
Kaunti za Maeneo Kame ya Ukanda wa Kaskazini mwa nchi zimeendelea kuishinikiza serikali kuwapa Kima cha Shilingi bilioni 14 kutoka kwa Hazina ya Usawazishaji inayozuiwa na Wizara ya Fedha. Wakizungumza baada ya kuipokea kaunti ya Pokot Magharibi kwenye mkutano wa baraza la maendeleo ya kaunti hizo mjini naivasha, walitoa wito mpya wa kutolewa mara moja kwa fedha hizo ili kuendeleza maendeleo.