10th July, 2018
Wafungwa katika Jela la Shimo la Tewa wameelezea kutamaushwa na mwendo wa pole unaochokuliwa na Mamlaka husika kuwapa msamaha utakaowawezesha kuachiliwa huru. Wanasema ni takriban wafungwa mia mbili tu ndio wameachiliwa huru katika mpango huo wa kutoa msamaha katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. Wafungw hao walikuwa wakizungumza katika mkutano wa kusikiliza maombi ya msamaha ulioandaliw na kamati ya kutoa msamaha kwa wafungwa. Jela la shimo la tewa lina idadi ya zaidi ya wafungwa alfu nne.