3rd July, 2018
Gavana wa kaunti ya Busia Sospeter Ojaamong amesema kwamba madai ya ufisadi dhidi yake ni ya uongo .Ojamoong anasema kwamba hajapokea ilani yoyote ya kushtakiwa kwake kwa madai ya ufisadi katika kaunti hiyo . Mkurugenzi wa mashtaka ya umma Noordin Hajj. aliidhinisha kufunguliwa mashtaka dhidi ya gavana huyo kwa madai ya matumizi mabaya ya mamlaka. Inadaiwa kuwa Ojaamong alikiuka kanuni za utoaji zabuni na hivyo kuisababishia kaunti ya Busia kupoteza mamilioni ya pesa.