2nd July, 2018
Wanaume wa matabaka mbali mbali kutoka jamii ya wamaasai wamekubaliana kwa kauli moja kuwaunga mkono viongozi wanawake katika jamii hiyo. Wakizungumza katika hafla ya kumvisha kofia ya uchifu Bi. Mary Rakita wanaume hao walijilaumu ni kwa nini hawakuwapa nafasi wanawake tangu kitambo ili walete maendeleo kupitia mbinu zao adimu za kuiongoza jamii. aidha waliongeza kuwa hawataona haya kupeleka kesi zozote hata zile za mizozo ya nyumbati kwa machifu wa kike ili zisikizwe na kuamuliwa vilivyo.