29th June, 2018
Waziri wa elimu daktari Amina Mohamed ameonya dhidi ya udanganyifu kwenye mitihani ya taifa mwaka huu. Waziri amewatahadharisha walimu na wanafunzi wanaopanga uovu huo kwenye mitihani ya kcpe na kcse mwaka huu, kwamba wataadhibiwa vikali. Alizungumza huko Eldoret.