21st June, 2018
Mkurungenzi wa shirika la kukadiria ubora wa bidhaa nchini KEBS Charles Ongwae ameiambia kamati ya bunge kuhusu kilimo kwamba maafisa wake hawakupata ushahidi wowote wa sumu katika sampuli ya sukari iliyowasilishwa katika maabara yake. Ongwae amesema sukari yote inayoagizwa hukaguliwa inakotoka na cheti cha uhalali na ubora kutolewa.