.
19th June, 2018
Jamaa mmoja amedungwa kisu na kuuawa maeneo ya Kamulu kwa kukosa kulipa chakula cha shilingi hamsini kwenyekibanda kimoja. Inadaiwa mwenye kibanda hicho kwa usaidizi wa mkewe walimvamia jana usiku na kumdunga kisu jamaa huyo aliyekosa kulipa shilingi hamsini baada ya kula githeri . Wenyeji wa eneo hilo waliojawa na gadhabu walivamia kibanda hicho na kukiteketeza huku wakitishia kulemaza biashara iwapo polisi hatawakamata wahusika hao wawili. Maafisa wa usalama waliuchukua mwili wa mwathiriwa na kuupeleka katika chumba cha kuhifadhia maiti.