13th June, 2018
Mwakilishi wa kike katika kaunti ya Nairobi Esther Passaris amevitaka vyombo vya ujasusi kuzichukua fedha na mali kutoka kwa wanaoshukiwa kuiba mali ya umma Passaris amesema kwamba fedha nyingi zilizoibwa kutoka kwa idara za serikali kama vile NYS zingesaidia kuleta maendeleo mashinani . Passaris aliyekuwa akizungumza katika eneo la Babadogo jijini Nairobi amesema kuwa wafisadi hawafai kuruhusiwa kusherehekea mali ya umma .