13th June, 2018
Jopo litakalojumuisha mashirika mbali mbali limebuniwa kuwasaidia waathiriwa wa mkasa wa kuporomoka kwa bwawa la Patel katika eneo la Solai kaunti ya Nakuru kurejelea maisha yao ya kawaida. Bwawa hilo lilivunja kingo zake mwezi mmoja uliopita na kusababisha vifo vya watu 47 na kuacha uharibifu mkubwa wa mali kundi la maafisa kutoka serikali ya kaunti likiongozwa na gavana Lee Kinyanjui na kamishna wa jimbo hilo Mongo Chimwanga limewaambia waathiriwa wa mkasa huo kwamba wote watapigwa msasa ili kukadiria wanaohitaji msaada