8th June, 2018
Kaunti ya Nairobi mapema hii leo imewatia mbaroni wachuuzi kwenye soko la City Market mkurugenzi wa utekelezaji Peter Mbaya amesema oparesheni hio inanuia kuwanasa wafanya biashara wasio na leseni kutoka mamlaka husika jambo analitaja kama hatari kubwa kwa wakaazi wa Nairobi. Mbaya amesema oparesheni hio itaendelezwa kwenye masoko ya Kariakor na Burma. Wachuuzi hao wamelalama kwamba walidhulumiwa wakati wakitiwa mbaroni.