7th June, 2018
Wamiliki wa baa katika kaunti ya Embu wameteta kunyanyaswa na maafisa wa serikali wanaofanya uchunguzi kwa wale wanaokiuka sheria za matumizi ya vinywaji haswa vileo. Wamiliki hao wameteta maafisa wa NACADA, KEBS na wale wa KRA wanafanya kazi isiyo yao kwani jukumu la kutoa leseni kwa wahudumu wa baa zinatolewa na serikali za kaunti.