.
5th June, 2018
Magunia 1474 ya sukari haramu yamepatikana katika mtaa wa Easleigh pamoja na mitungi 504 ya lita 20 ya mafuta haramu. Hii ni kwa mujibu wa inspekta mkuu wa polisi Joseph Boinnet ambaye amesema haijulikani mizigo hiyo imetoka nchi gani huku akiripoti kukamatwa kwa watu watatu kwa kushukiwa kuhusiaka. Aidha amedhibitisha uchunguzi umeanza huku vipimo vya bidhaa hizo vikichukuliwa kubaini iwapo ni salama kwa matumizi na binadamu.