5th June, 2018
Waziri wa elimu Amina Mohammed ameamrisha kuvunjwa kwa bodi ya shule ya upili ya Moi Girls baada ya msichana mmoja kuthibitrishwa kubakwa katika shule hiyo. Wakati huohuo mwalimu mkuu wa shule hiyo Joel Mureithi ameamua kustaafu kutokana na suala hilo . Waziri Amina alitoa maagizo hayo wakati wa mkutano na wanahabari ambapo pia alitoa amri ya kuimarishwa kwa usalama nje ya shule hiyo.