4th June, 2018
Wanawake wa Murang’a Kusini wanaongoza katika biashara ya kuuza bangi. Hii ni kwa mujibu wa naibu kamishina wa eneo hilo Titus Macharia. Macharia hata hivyo ameteta kwamba wanawake hao wanapofikishwa mahakamani wanatozwa faini ndogo mno na hivyo kutaja vita dhidi ya mauzo ya bangi vinakumbwa na matatizo mengi. Akizungumza huko Kamahuha pia amesema matumizi ya pombe ni ya kiwango cha juu na kutaja kuwa maeneo ya kutengeneza pombe ni mengi mno kuzidi shule.