2nd June, 2018
Mwanahabari shupavu wa KTN Sycilia Mzae Wakesho hii leo amefunga pingu za maisha na mpenziwe Moses Mathuva. Sherehe hiyo ya harusi ilifanyika katika kanisa la Kianglikana la All Souls Cathedral huko Machakos. Maharusi hao baadaye waliandamana na wazazi, ndugu na marafiki kwa karamu murwa kabisa ya chakula na kukata keki katika bustani la Machakos Golf Club. Hongera sana kwa bwana na bi Mathuva na nawatakia kheri njema wanapoanza safari yao ya maisha pamoja.