27th May, 2018
Kiongozi wa mashtaka ya umma Nordin Hajji amepokea faili kumi ambazo zina mapendekezo ya kufunguliwa mashtaka kuhusiana na sakata ya shilingi bilioni 9 katika idara ya huduma ya vijana NYS. Faili hizo zinajumuisha kampuni 10 na watu zaidi ya 40. Haya yanajiri huku naibu rais William Ruto akionya asasi za kupambana na ufisadi kuwajibika na kuhakikisha wahusika wanachukuliwa hatua kali.