27th May, 2018
Viongozi kutoka eneo la Rift Valley wameendelea kunyosheana kidole cha lawama kuhusiana na sakata ya mahindi ambapo orodha ya watu 18 ilitolewa kwa madai kwamba waliifilisi NCPB. Kesho panatarajiwa maandamano ya wakulima mjini Eldoret ambapo mbunge wa Nandi Hills Alfred Keter ameapa kuyaendesha licha ya kuonywa na baadhi ya viongozi wa Rift Valley.