26th May, 2018
Naibu kiongozi wa wachache kwenye bunge la Seneti, Cleophas Malala, ametoa mwito kwa wanachama wa kamati za bunge zinazohusika na masuala ya uhasibu kumuagiza gavana wa Kirinyaga Anne Waiguru kufika mbele ya kamati hizo kujibu maswali kuhusu sakata ya NYS. Malala anasema Waiguru anastahili kuwajibika kwa vile kashfa ya uporaji wa mali ya umma ilifanyika kwenye idara hiyo alipokuwa akihudumu kama waziri. Aidha, Malala pia amewataka wabunge wa kaunti ya Kirinyaga kuwasilisha mswada wa kumuondoa Waiguru afisini.