25th May, 2018
Kwingineko katika kashfa ya NCPB, seneta wa Baringo Gideon Moi amemtaka Rais Uhuru Kenyatta kuwachukulia hatua kali wanaohusika na ufisadi katika kashfa hiyo ambayo ni ya kima cha shilingi bilioni moja nukta tisa. Gideon amesema kuwa mara nyingi viongozi kutoka maeneo ya Rift Valley wamekuwa wakitaka serikali kuwashughulikia wakulima na badala yake baadhi ya wakuu wa NCPB wakishirikiana na wakulima fulani walikuwa wakiwapunja wakulima, na hivyo kukaa muda mrefu bila kulipwa. Gideon ametoa wito kwamba wakulima walipwe fedha zao huku uchunguzi ukiendelea. Ujumbe wa Gideon umeungwa mkono na baadhi ya wabunge wa Jubilee ambao wamesema kuwa ni sharti Rais Kenyatta awajibike na kuhakikisha kuwa wahusika katika kashfa za NYS na NCPB wanakabiliwa vilivyo kisheria.