×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Wakazi West Pokot waandamana; wasema naibu gavana amezembea kazini

25th May, 2018

Baadhi ya wakazi wa West Pokot wamemtaka naibu wa gavana katika kaunti hiyo kujitokeza kwani hawajamuona kwa miezi mingi. Wananchi  hao  aidha wanamlaumu gavana John Lonyangapuo kwa kuwa hajachukua hatua yoyote baada ya naibu wake Nicholas Atudonyang kutoonekana. Wanasema kutoweka kwake kunapelekea ukosefu wa huduma zinazotegemea afisi yake na kukosekana kwa maenedeleo. Wameapa kwamba watafanya maandamano hivi karibuni kushinikiza hatua kuchukuliwa dhidi ya Atudonyang ambaye pia anasimamia sekta ya afya katika kaunti ya West Pokot kama waziri. Msaidizi wa naibu gavana James Kodoso amesema kuwa gavana John Lonyangapuo anafahamu fika alipo naibu wake na kwamba majukumu yake yanatekelezwa.

 

.
RELATED VIDEOS