21st May, 2018
Wengi huwa na dhana kwamba ugonjwa wa saratani huwa ni tiketi ya kifo. Lakini sio kwa daktari Catherine Nyongesa ambaye sasa anajivunia kuwa na mojawapo ya kituo kikuu cha kutibu saratani sio tu nchini bali barani Afrika. Kwenye makala ya mwanamke ngangari leo hii mwanahabari Sycilia Wakesho anaangazia safari ya mwanamke ambaye mtazamo wake kuhusiana na tiba ya saratani ulibadilika baada ya juhudi zao za kumtibu dadake saratani kufanikiwa.