15th May, 2018
Hatimaye Gor Mahia watachuana na Usm Alger kutoka Algeria katika uga wa Moi sports center Kasarani. Awali kulikuwa na taarifa kwamba Kogalo hawatachezea uga huo baada ya baadhi ya mashabiki wake kuharibu mali katika mchuano wao na Hull City. Hata hivyo katibu wa wizara ya michezo balozi Peter Kaberia hatimaye ametoa afueni hii kwa mashabiki wa vigogo hao wa soka nchini.