.
8th May, 2018
Habari zinazotufikia kutoka eneo bunge Tiaty ni kwamba ugonjwa ambao haujulikani umewaua watu wanane katika kijiji cha Lodeng'o kata ya Kolowa. Ugonjwa huo ambao dalili zake ni kuharisha, kutapika, maumivu ya tumbo umesababisha hofu katika sehemu hiyo muuguzi mkuu wa kituo cha afya cha Lodeng'o Clara Lotuw akidokeza kwamba sampuli za chembechembe zimepelekwa kwa uchunguzi maabarani