1st May, 2018
Shughuli za usafiri kwenye barabara ya Githunguri zilisitishwa kwa muda baada ya wakazi kuandaa maandamano. Mamia ya wenyeji walijitokeza kulalamikia ubovu wa barabara hiyo kutoka Githunguri hadi Kimende licha ya ahadi za serikali kuwa itatengenezwa. Wakazi hao waliojawa na hamaki waliwasha mioto kwenye barabara hio na hatimaye kuandamana hadi kwa ofisi ya Mbunge wa eneo hilo kutoa lalama zao