27th April, 2018
Gavana wa Elgeyo Marakwet Alex Tolgos amelaumiwa na baadhi ya waakilishi wadi katika kaunti hiyo kwa kile wanachokitaja kuwa ukosefu wa uwakilishi wa kutosha katika kongamano la ugatuzi lililokamilika hapo jana mjini Kakamega. Wamelalama kuwa kaunti hiyo ndiyo kaunti pekee ambayo haikushiriki kwenye kongamano hilo ambalo lilifanywa kwa mwaka wa tano tangu kuanza kwa utawala wa magatuzi kwa mujibu wa katiba ya nchi.