24th April, 2018
Timu ya Tusker Fc imezindua Robert Matano kama kocha wake mpya baada ya kutimuliwa kwa aliyekuwa mkufunzi Sam Timbe siku ya Jumapili baada ya msururu wa matokeo duni.Matano atachukua usukani mara moja huku akinuia kuandikisha ushindi dhidi ya timu ya Wazito Fc siku ya Jumatano huku lengo lake kuu likiwa ni kuimarisha matokeo ya Tusker pamoja na kuiwezesha kumaliza katika nafasi bora ligini.