23rd April, 2018
Mwanamuziki mashuhuri wa lingala Nyboma Wwan'dido kutoka nchini Congo DRC amewasili nchini kwa mwaliko wa muungano wa vyama vya wafanyikazi nchini COTU. Nyboma alipokelewa jana usiku katika uwanja wa ndege wa JKIA na katibu wa COTU Francis Atwoli. Nyboma amekuja kutumbuiza kwenye sherehe za Leba Dei hapo Mei tarehe moja