23rd April, 2018
Wachezaji raga wawili wanaodaiwa kumbaka mwanamuziki mmoja humu nchini wamefikishwa mahakamani na kushtakiwa kwa ubakaji.Lawrence Frank Wanyama na Alex Mahaba Olaba walisomewa mashtaka ya ubakaji wa zamu tarehe 11 Februari mwaka huu mbele ya hakimu mkuu wa Nairobi Francis Andayi. Wawili hao wanashtakiwa kwa kufanya kitendo hicho katika jumba la Seefa eneo la Highrise. Wameachiliwa kwa dhamana ya shilingi laki tano kila mmoja na kesi itasikizwa tarehe 16 mwezi ujao.