22nd April, 2018
Watu wanane wamefariki kufuatia ajali ya barabarani katika eneo la Kyumbi kwenye barabara kuu ya Nairobi Mombasa.Ajali hiyo ilitokea mwendo wa saa nane alfajiri ya leo wakati matatu iliyokuwa ikisafiri kutoka eneo la loitoktok iligonga lori lililokuwa limeegeshwa. Abiria wengine wanne wamejeruhiwa vibaya na kukimbizwa
hospitalini kwa matibabu.