20th April, 2018
Mwenyekiti wa tume huru ya uchaguzi na mipaka Wafula Chebukati amejitetea dhidi ya madai yaliyoibuliwa na makamishna watatu wa IEBC waliojiuzulu mapema wiki hii akisema ni ya kupotosha na kupaka tope jina lake. Chebukati pia ameelezea kuhusu mkutano wa tume yake na kamati ya bunge la seneti kuhusu masuala ya sheria, mkutano uliokosa kufanyika mapema leo kuangazia matukio kwenye tume hiyo.